NYAKATI ZA UDANGANYIFU – TAHADHARI!
SOMO: NYAKATI ZA UDANGANYIFU – TAHADHARI!
"Maana watu wengi wadanganyaji wametokea duniani..."(2 Yohana 1:7)
Katika nyakati hizi, dunia imejaa utapeli na udanganyifu. Watu huvaa sura za upole, lakini ndani ni mbwamwitu. Wanaweza kujifanya wapendanao, wachungaji, marafiki, au hata “watu wa Mungu” – kumbe ni wanyang’anyi wa roho na hisia zako!
AINA 4 ZA UTAPELI WA NYAKATI HIZI:
1. Mapenzi ya Kijanja:
Wanaandika "I love you", lakini lengo ni kukutumia.
“Kwa maana midomo yao hunena amani na mioyo yao huwaza mabaya.”
— Zaburi 28:3
2. Utapeli wa Kifedha:
Wanaahidi biashara au misaada, kumbe wanapanga kukuibia.
“Asiyefanya kazi na asile.”
— 2 Wathesalonike 3:10
3. Udanganyifu wa Kiimani:
Manabii wa uongo wanahubiri mafanikio bila wokovu.
“Kwa sababu watajitokeza manabii wa uongo... wapate kuwapoteza hata wateule.”
— Mathayo 24:24
4. Marafiki wa Kuumiza:
Wanajifanya wako karibu, lakini huleta chuki, fitina na wivu.
“Yeye ajifanya rafiki lakini moyo wake hujawa na hila.”
— Methali 26:24
USHAURI KWA WANAOMJUA MUNGU:
> “Jihadharini, msidanganyike: Mungu hadhihakiwi...”Wagalatia 6:7
Mwamini wa kweli anahitaji roho ya utambuzi (discernment).
Usiongozwe na hisia – omba hekima!
WITO KWA WASIO MJUA MUNGU:
“Tazama, sasa ni wakati wa kupendelewa; tazama, sasa ndiyo siku ya wokovu.”
2 Wakorintho 6:2
Kabla hujatapeliwa kwa upendo au pesa, tafuta upendo wa kweli kwa Mungu. Dunia haina hakikisho, lakini Yesu yupo tayari kukulinda na kukuongoza.
HITIMISHO:
"Wote waongozwao na Roho wa Mungu, hao ndio wana wa Mungu." Warumi 8:14
Jifunze kusema HAPANA kwa udanganyifu, na NDIO kwa ukweli wa Neno la Mungu.
Usikubali mapenzi, pesa au maneno mazuri yakupofushe!
Imeandaliwa na:
Kisakenyi Mnzava
Mhubiri na Mwalimu wa Neno la Mungu
Mawasiliano:
WhatsApp/Simu: +255 764 317 590
Email: issacklucas2@gmail.com
#UjumbeWaLeo
#TahadhariNaUtapeli
#NenoLaMungu
#MahusianoYaKweli
#RohoYaUtambuzi
#MapenziYaKweli
#UtapeliWaKiroho
#UshauriWaKiBiblia
#MafundishoYaImani
#NyakatiZaMwisho
#ChristCentered
#Discernment
#RelationshipTruth
#TrueLoveNotScam
#BiblicalWisdom
#KingdomMindset
#BeWatchful
#SpiritualAlert
#Jihadhari
#UkweliWaNeno

Maoni
Chapisha Maoni