DALILI ZA KUJA KWA KRISTO NA MWISHO WA DUNIA – JE, UMEJIANDAA?

 DALILI ZA KUJA KWA KRISTO NA MWISHO WA DUNIA – JE, UMEJIANDAA?


MAANDIKO (Mathayo 24:3-14):

Yesu alikaa juu ya mlima wa Mizeituni, wanafunzi wake wakamjia faraghani wakisema:

"Tuambie, mambo hayo yatakuwa lini? Nayo ni nini dalili ya kuja kwako, na ya mwisho wa dunia?"

(Mathayo 24:3)


Yesu aliwajibu:


"Angalieni, mtu asiwadanganye. Wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, Mimi ni Kristo; nao watadanganya wengi." (aya 4-5)


"Mtasikia vita na matetesi ya vita... lakini mwisho bado." (aya 6)


"Kutakuwa na njaa, tauni, na matetemeko ya ardhi mahali mbalimbali. Lakini hayo yote ni mwanzo wa utungu." (aya 7-8)


Waumini watachukiwa, kusalitiwa, na kuuawa. (aya 9-10)


"Manabii wa uongo watatokea... upendo wa wengi utapoa." (aya 11-12)


"Lakini mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka." (aya 13)


"Tena habari njema ya Ufalme itahubiriwa duniani kote; ndipo ule mwisho utakapokuja." (aya 14)


UJUMBE WA KUTAFAKARI:

Je, dalili hizi hatuzioni leo? Vita, tauni, vifo, njaa, chuki, na upendo wa kweli kupoa? Huu ni wakati wa kumrudia Yesu, kuwa macho, na kueneza injili. Usingoje hadi mwisho ufike — jiandae sasa.


#YESUANAKUJA #MWISHOWANYAKATI #MATHAYO24 #INJILIYAKWELI #IMANINATUMAINI #BIBILIA


Imeandaliwa na: Kisakenyi Mnzava

Mwalimu wa Neno la Mungu na Mshauri wa Mahusiano

Pata mafundisho zaidi kupitia:

Facebook/TikTok/Instagram

Email: Issacklucas2@gmail.com

WhatsApp: +255 764 317 590

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KWANINI WATU WENGI LEO WANAABUDU WATU NA SIO MUNGU?

📖 HAKUNA MWANADAMU MKAMILIFU

KWANINI NIOGOPE SIKU ZA UOVU?